Matokeo ya mitihani ile yalipotangazwa moja kwa moja hewani, nilikuwa katika safu ya watahiniwa wachache waliokwagura alama takriban zote. Mtima wangu ulibopabopa kwa kiwewe cha bashasha bin liwazo kwani nilijua wazi kama mchana kuwa nyanyangu ataniezeka mkate mzima wa boflo. Boflo kijijini chetu ilikuwa nadra kama maji kwenye jangwa la Sahara na nilijua kuwa vijana majirani watataka kusherehekea na mimi pia ijapokuwa sherehe yao itakuwa ya boflo tu.Waliosema zawadi ni mbolea ya urafiki hawakupotoka hata kidogo.
No comments:
Post a Comment