Shabaha yangu ya kuendelea na masomo ilifika tamati. Kwa kuwa huwezi kutazamia tasa kuzaa au kuku kuyatoa maziwa, haya yalikuwa sawia nami kufikiri kuyaendeleza masomo yangu ilhali sikuwa na yeyote wa kunidhamini.
Maisha yangu yalikuwa ni kama yamewekewa alama ya kudonesha kwani niliyapenda masomo kupindukia. Nilichobakia nacho tu ni nguvu za kusadiki na kumpeperushia Mola sala zangu nyenyekevu nikitumai kwamba atanipa jawabu.