Tuesday, December 27, 2011

Kisa 1

Bila kubananga wakaa, ningependa kuwajulisha hili kwa muda mfupi uliosalia.

Palitukia banati mmoja katika kijiji chetu Kanyageni na mwili wake ulikuwa umelainika kama parachichi bivu. Maziwa yake yalisimama tisti boriti kifuani mwake. Mashavu yake yalijaajaa na yaliunda vidumbwi maridadi kila alipocheka. Maninga yake yalikuwa ya kikombe. Mdomo wake wa chini uliokuwa mkubwa kidogo kuliko wa juu uliyafanya meno yake yaonekane wazi kila alipoangua kicheko. Meno yake yalingaaa utadhani saluji.Vijana wengi walimtamania na vijana wengi walijaribu bahati yao.

Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuzama shimoni lile, jambo ambalo, kuzingatia utamaduni lilikuwa mwiko. Maziwa yalishaamwagika. Niliapa kutorudia jambo lile tena kwani maisha yangu yalishaakosa maana kwangu yakawa sampuli ya tupu la yai.

Nilikuwa nishaambukizwa ugonjwa mbaya wa ukimwi.